MAOMBI YA VITA

Maombi ya vita yakoje?..Je! ni lazima kuomba maombi ya vita?

Maombi yamegawanyika katika sehemu kuu 3

Maombi ya shukrani

Maombi ya kuwasilisha haja mbele za Mungu.

Na Maombi ya KUTANGAZA.

Katika aina aina ya kwanza ya maombi ni ile ya KUSHUKURU, Ambapo mwamini atapiga magoti au atasimama na kumshukuru Mungu kwa mema yote anayomtendea yeye binafsi, na familia yake, na jamaa zake, na Taifa lake…hali kadhalika na kwa kila kitu ambacho anastahili kukishukuru mbele za Mungu. Na maombi haya ndio maombi ya muhimu kuliko yote, na yanayopaswa kuchukua muda mrefu kuliko maombi mengine yoyote.

Aina ya pili ya maombi ni ya kuwasilisha haja mbele za Mungu…Haya ni yale ambayo mtu atapiga magoti na kumwomba Mungu hitaji fulani amtimizie, hilo linaweza kuwa hitaji lake binafsi au la mtu mwingine au la kanisa au la Taifa.

Na Aina ya tatu na ya mwisho ya maombi ni maombi ya KUTANGAZA…Katika aina hii ya mwisho ya maombi ndipo panapopatikana maombi ya vita kama yanavyotajwa na wengi, yanaangukia katika kundi hili.

Katika maombi ya kutangaza..hapa ndipo mtu atatumia kinywa chake na mamlaka aliyopewa kuamuru na kuamrisha kila nguvu zote za giza, zilizo kinyume na nguvu za Mungu zipate kuanguka chini kwa jina la Yesu..

Mfano wa maombi ya kutangaza ni maombi ya kutoa pepo. Tunapoamuru pepo amtoke Mtu au kitu kwa jina la Yesu hapo tumetangaza kile kitu kifunguliwe kwa mamlaka ya kimbinguni, na hivyo ni lazima kitii.

Hali kadhalika kama kuna maneno maovu, au mitego ya adui, au kuna mipango na mikakati iliyopangwa na wanadamu au watumishi wa shetani dhidi yako au ndugu,au jamaa au kanisa au Taifa, kwa kutumia vinywa vyetu na kwa jina la YESU, tunaweza kuifuta mipango hiyo, na ratiba hizo na mikakati hiyo, na ikafutika sawasawa na tulivyotamka/kutangaza.

Sasa maombi haya ndio yanayojulikana na wengi kama MAOMBI YA VITA..Mwamini anaweza kutumia muda wa kutosha kutamka baraka juu yake na kwa ndugu zake na kwa kanisa la Kristo kwa jina la Yesu, hali kadhalika anaweza kutangaza kufuta kila mipango ya ibilisi iliyopangwa juu yake, juu ya familia yake, ndugu zake, kazi zake, afya yake, kanisa lake, nchi yake na kila kitu kinachohusiana na yeye. Maombi haya yanaweza kuchukua masaa kadhaa kwa kadiri mtu alivyojaliwa kuomba, na yanaweza kufanyika kila siku. Na pia ni maombi ya muhimu sana. Na maombi haya yanahusisha kutoa au kupaza sauti kwa nguvu…Huwezi kukemea pepo lililopo ndani ya mtu kimoyomoyo…Katika biblia Bwana wetu Yesu, pamoja na Mitume walitamka kwa nguvu na pepo wakawatoka watu…Bwana alipoulaani ule mtini, alitoa sauti kutoka katika kinywa chake..Hali kadhalika tunapozilaani kazi za Adui shetani, ni lazima sauti zitoke katika vinywa vyetu. Sio lazima itoke sauti kama kilio, lakini angalau sauti isikike..Na ndivyo shetani na mapepo yake tutakavyoyaangusha chini..

Maombi haya hayana muda maalumu wa kuomba…Ni vizuri zaidi kuomba kwa pamoja kama kikundi, au peke yako binafsi wakati wa utulivu.

Bwana akubariki.

Axact

Tanzania Worships

Haleluyah! Karibu katika ukurasa wa Tanzania Worships ambao ni maalumu kwa ajili ya kusambaza na kulihubiri Neno la Mungu anayeishi. je kuna maoni na ushauri unataka kuuutoa ili kuhakikisha ukurasa huu unawafikia waamini na wasioamini? basi usione shaka kuwasiliana nasi kwa njia ya mitandao ya kijamii

Post A Comment:

0 comments: