*Kwanini Tunafunga*
Kufunga ni zoezi la Kiroho, lenye sababu na faida nyingi.  Kabla ya hizo, jua kwamba Mungu anakutarajia uwe unafunga kula.

*Mathayo 6:16*
Tena -mfungapo-, msiwe kama wanafiki wenye uso wa kukunjamana; maana hujiumbua nyuso zao, ili waonekane na watu kuwa wanafunga. Amin, nawaambia, wamekwisha kupata thawabu yao.

"Tena mfungapo" ikimaanisha "mtakapofunga". Hivyo inatarajiwa kuwa utakuwa mtu wa kufunga.

Kwa Kiingereza, imewekwa vizuri zaidi. Imeandikwa *when you fast* (utakapofunga) na sio *if you fast* (sio ikiwa utafunga). Hivyo Mungu ankutarajia uwe unafunga kula.

*Sababu za Saumu*
1. Inashoodisha mwili (the body) na mambo yake (the flesh - tamaa, hamu, haja) *Rum 8.5-11

2. Inahuisha Roho yako. 
Gal 5.16-21

3. Inakunyenyekesha mbele za Mungu. 2Fal 22.19, 2Nyak 7.14, 2Nyak 36.12

4. Inakupa mpenyo mzuri katika kumtafuta BWANA *Yer 29.12-13, Zab 35.13, Matendo 13.1-3

5. Inapika kiwango cha lmani
Math 17.19-21,

6. Kuachilia kiwango cha Nguvu za Mungu
Isa 58.6, Luk 4.1-4, 14, 18-19, Marko 1.21-34

7. Inasafisha mwili. Mafuta, sukari, uchafu kwenye damu na seli. Kwakuwa mwili hauna kazi ya kumeng'enya chakula, basi mwili unapata muda kufanya usafi. Ndio maana baada ya kufunga, *afya inakurudia*
Isaya 58.8

*Mwl. Mgisa Mtebe*
*+255753497655*

Instagram: @mgisamtebe
YouTube: Mgisa Mtebe
Facebook (Page): Mgisa Mtebe

Axact

Tanzania Worships

Haleluyah! Karibu katika ukurasa wa Tanzania Worships ambao ni maalumu kwa ajili ya kusambaza na kulihubiri Neno la Mungu anayeishi. je kuna maoni na ushauri unataka kuuutoa ili kuhakikisha ukurasa huu unawafikia waamini na wasioamini? basi usione shaka kuwasiliana nasi kwa njia ya mitandao ya kijamii

Post A Comment:

0 comments: