Bwana Yesu asifiwe wapendwa,leo tunaanza mada nyingine mpya juu ya majaribu ama kwa kiingereza (Temptations).Tumesoma maranyingi sana kwenye maneno ya Mungu kuhusu majaribu na tumeona namna watumishi wa Mungu walivyokuwa wakijaribiwa na wengine kuzama kwenye mitego hiyo ya majaribu.

Ukiwa kama mtumishi wa Mungu,majaribu ni lazima yakupate,kiuharisia jaribu ni changamoto ambazo lazima ukutane nazo katika safari yako ya imani,hazikimbiliki kabisa. Yesu alijaribiwa pia alipokuwa duniani ili kutuonyesha yatuoasayo kuyafanya kipindi tupitapo kwenye majaribu.

Kuna kitu kingine ambacho wengi tunakichanganya wengi tunaamini jaribu ni lazima mtu upate shida fulani,ama magonjwa,kuyumba kiuchumi nk,hii dhana haipo sahihi sana,kuna aina ingine ya majaribu ambayo haihusiani na mambo hayo kabisa. 

Basi tuanze kuangalia mambo ya msingi,naamini baada ya kipindi hiki,maswali mengii  kuhusu majaribu tutakuwa tumeyajibu. Amen


AINA ZA MAJARIBU

Kuna aina kuu mbili za majaribu ambayo tunayapitia katika maisha ya wokovu.

1. KUJARIBIWA KWA KUFANYA MAOVU

Tutachukua muda mwingi kuzungumzia aina hii ya kujaribiwa.Hivyo vipengele vitakavyofuata (maana ya jaribu,vyanzo vya majaribu,aina mbali mbali za kujaribiwa kwa maovu,jinsi ya kushinda majaribu) vyote vitakuwa vinazungumzia aina hii ya majaribu NB; KUARIBIWA KWA MAOVU HAKUTOKANI NA MUNGU.

 YAKOBO 1:13   - Mtu ajaribiwapo, asiseme, Ninajaribiwa na Mungu; maana Mungu hawezi kujaribiwa na maovu, wala yeye mwenyewe hamjaribu mtu. Lakini kila mmoja hujaribiwa na tamaa yake mwenyewe huku akivutwa na kudanganywa.
Kujaribiwa kwa maovu ni tendo la kumvuta na kumdanganya mtu ili ikiwezekana mtu huyo atende dhambi (YAKOBO 1:14-15). Kujaribiwa sio dhambi,ila kuingia kwenye namna hii ya majaribu na kuvutika mpaka kufanya uovu ndio dhambi.
Hata Bwana wetu Yesu kristo alijaribiwa kwa namna ya majaribu kama haya na shetani alipokuwa kwenye mfungo,lakini kamwe hakutenda dhambi 

Kwa kuwa hamna kuhani mkuu asiyeweza kuchukuana nasi katika mambo yetu ya udhaifu; bali yeye alijaribiwa sawasawa na sisi katika mambo yote, bila kufanya dhambi.
EBR. 4:15
Kama Bwana Yesu alijaribiwa kwa namna hii na yeye ndiye kinara wetu na mwongoza njia yetu,basi kila amwaminiye Yesu,yampasa kutambua kuwa majaribu yatakuja kwake kwa namna za tofauti (Rushwa,uzinzi,uongo nk) lakini yampasa kuyashinda kama Yesu alivyishinda.


VYANZO VYA MAJATIBU YA NAMNA HII..

Tumeona kwenye kitabu cha yakobo kuwa Mungu hafanyi majaribu ya namna hii,inamaana moja kwa moja shetani anahusika.
Tunakumbuka katika bustani ya Edeni vile alivyohusika kuwadanganya watu wa Mungu,alivyotaka kumdanganya Yesu nk. Kwa hiyo,majaribu ya namna hii,chanzo ni shetani na malaika zake.

Kwa hiyo mimi nami nilipokuwa siwezi kuvumilia tena, nalituma mtu ili niijue imani yenu, asije yule mjaribu akawajaribu, na taabu yetu ikawa haina faida.
1 THE. 3:5 
Lakini nachelea; kama yule nyoka alivyomdanganya Hawa kwa hila yake, asije akawaharibu fikira zenu, mkauacha unyofu na usafi kwa Kristo.
2 KOR. 11:3
Mjaribu anayezungumziwa hapa ni shetani.pia kasome (MATHAYO 4:1,3:1)

Pia shetani huwatumia wanadamu ili kuleta aina hii ya majaribu. Alimtumia delila,alimtumia Yuda ili kuingiza haya majaribu kwa watu wa Mungu.

Wakatokea Mafarisayo, wakaanza kuhojiana naye; wakitafuta kwake ishara itokayo mbinguni; wakimjaribu.
MK. 8:11
Pia tamaa za mwili wa mtu mwenyewe zinaweza zikafanya akaingia kwenye haya majaribu.miili yetu hutumia na shetani ili kutujaribu na ndio maana mara kwa mara inabidi tuwe tunaombea milango yetu mitano ya fahamu na kuikomboa kwa damu ya yesu ili mwovu aiweze kuitumia kwa kuyujaribu au kutuingiza majaribuni.

(YAKOBO 1:14)

Kwahiyo,aina hii ya kujaribiwa ndio aina kuu ya majaribu ambayo yanatupasa kuyashinda.

Katika sehemu inayokuja tutaangalia aina hii ya ya majaribu na mifano yake pia na njia za kuyashinda haya majaribu.jina la BWANA libarikiwe.
Axact

Tanzania Worships

Haleluyah! Karibu katika ukurasa wa Tanzania Worships ambao ni maalumu kwa ajili ya kusambaza na kulihubiri Neno la Mungu anayeishi. je kuna maoni na ushauri unataka kuuutoa ili kuhakikisha ukurasa huu unawafikia waamini na wasioamini? basi usione shaka kuwasiliana nasi kwa njia ya mitandao ya kijamii

Post A Comment:

0 comments: