🌱Tzworships bible study
 #Kitabu cha mwanzo.

 Tunapoenda kuangalia kitabu cha mwanzo,naomba nikukumbushe kitu kidogo ambacho alikisema yesu juu ya Musa. Kitu hiki kinapatikana katika *YOHANA* 5:46 ,Yesu anasema kuwa Musa aliandika kuhusu habari zake. Kumbe kila kitu alichokiandika Mussa kilimuhusu Yesu na Kitabu cha Mwanzo aliandika Mussa. Kuna mambo mengi ya kuangalia katika kitabu cha mwanzo,ila tutajikita zaidi katika muonekano wa Yesu katika kitabu cha mwanzo. Physical appearance of jesus. Kwahiyo katika Mjadala huu,tutaenda kuangalia ni jinsi gani Yesu anaonekana kwenye Mwanzo 1.

 Leo tutaangalia MWANZO 1:1-5 Ni maneno madogo ila yanamaana kubwa TUTAJIKITA HAPA KWA LEO Kwanza kabisa Kitabu cha mwanzo maana yake ni mwanzo,ama kwa kiingereza wanaita genesis ikimaanisha mwanzo wa vitu. Kitabu cha mwanzo pia ni mwanzo wa mambo mengi sna na ndiyo msingi wa imani yetu kiujumla. Genesis ni mwanzo wa dunia,mwanzo wa mbingu,mwanzo wa uhai na wanadamu,mwanzo wa dhambi na pia kitu kikubwa ambacho tutakuja kukiangalia katika kitabu cha mwanzo ni ukombozi ama redemption.Kitabu hiki pia ni mwanzo wa ukombozi wetu. Pia bila shaka naamini kuwa unafahamu sasa kuwa Mussa ndiye aliyeandika kitabu cha mwanzo.

Katika agano jipya,kuna kitabu kimoja tu ambacho maneno yake yanaanza kama kitabu cha mwanzo kinavyoanza "HAPO MWANZO" Kitabu hiko ni YOHANA MTAKATIFU. Nafahamu kuwa unafahamu kwamba Mungu ndiye muumba wa kila kitu,kinachoonekana na kisichooneka,maji na mchanga,mapepo na malaika..vitambaavyo vyote ni mkono wa Mungu ulifanya ivyo,ila kiuharisia zaidi tukiingia ndani,ni Yesu aliyafanya hayo yote kwa mikono yake kama moja ya nafsi katika utatu wa Mungu yaani Mungu Baba,mwana na Roho mtakatifu na Yesu akiwa nafsi ya Pili yaani Mungu mwana.🌚🌚

ushahidi wa haya ni huu hapa "Kwa kuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi, vinavyoonekana na visivyoonekana; ikiwa ni vitu vya enzi, au usultani, au enzi, au mamlaka; vitu vyote viliumbwa kwa njia yake, na kwa ajili yake." *KOL. 1:16* "Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu. Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu. Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika."

*YOHANA. 1:1‭-‬3* Kumbe Yesu alituumba mm na wewe kwa ajiri yake yeye mwenyewe,hii haina ubishi. Je,aliumba kwa kutumia nini.? soma hapa mwana tzworship "Kwa imani twafahamu ya kuwa ulimwengu uliumbwa kwa neno la Mungu, hata vitu vinavyoonekana havikufanywa kwa vitu vilivyo dhahiri." EBR. 11:3 Kumbe ni kwa imani tu,NENO lilifanya haya yote. Hii inanikumbusha andiko moja katika kitabu cha muhubiri linasema NENO LA MFALME LINA NGUVU Kila kitu kilifanywa kwa vitu visivyoonekana,kila unachokiona kilifanyika kwa visivyoonekana Watu wengi tunaamini kuwa hatuna kitu cha kumpa Mungu,tunasahau kuwa huyu Mungu aliumba kila kitu kutoka kwenye hamna. Kumbe anaweza kutumia hamna yako iyo ili afanye kitu.

 From nothing God created everything and he is the same God who can turn your nothing to something,just beliveeee. amini tuuuuu MWANZO 1:1 Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi. Nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu, na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji; Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji. MWA. 1:1‭-‬2 NA IWE NURU.... KWENYE MAISHA YAKO MWANZO 1:2-5 "Nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu, na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji; Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji. Mungu akasema, Iwe nuru; ikawa nuru. Mungu akaiona nuru, ya kuwa ni njema; Mungu akatenga nuru na giza." MWA. 1:2‭-‬4

 Nikitu cha kushangaza kuwa hii dunia hapo mwanzo ilifunikwa na maji,si ndio? na kwa usahihi kabisa tembelea ZABURI 104:5-9 Kwa leo tuangazie kidogo upande mwingine wa mistari hii na tuache hiki kisehemu cha maji. MUNGU AKASEMA IWE NURU NA IKAWA NURU NA AKAONA NURU NI NJEMA. Kabla ya yote Mungu aliumba kwanza nuru. He created light before anything,na Nuru ni ishara au ni Muonekano mwingine wa kristo. Kumbe kama Baba alifanya hivyo sisi ni zaidi. Dunia ilikuwa giza,Mungu akaleta kwanza Nuru kabla ye vyote ndipo akaanza kufanya vingine. Je unadhani Mungu alikuwa haoni mpaka akahitaji Nuru? na ukumbuke ni Nuru na sio mwanga? Mwanga huletwa na jua ila Nuru ni ya milele na haihitaji jua na ndio maana hata kabla Mungu hajaumba jua bado tulikuwa na mchana na usiku...AMAZIIIIIIING GOD🤷‍♂️

 Kumbe na sisi kabla ya vyote,kabla ya kufanya kitu chochote lazima tuumbe kwanza Nuru,Yesu kwanza na mengine yanafuata....hapa wametuzidi wapagani... FREEMANSON KWANZA halafu wanafanya mambo yao ila sisi tunafeli wapi sijui... Kwa kuwa Mungu, aliyesema, Nuru itang’aa toka gizani, ndiye aliyeng’aa mioyoni mwetu, atupe nuru ya elimu ya utukufu wa Mungu katika uso wa Yesu Kristo. 2 KOR. 4:6 TUPO PAMOJA???

Na sisi kabla ya kumjua Yesu tulikuwa watupu na giza,lakini Roho wa Mungu bado alikuwa anatuzungukia kama siku za uumbaji wa Dunia,Wokovu unapotujia ni Mungu anakuwa anaamuru Nuru iingie kwenye maisha yetu. uwafumbue macho yao, na kuwageuza waiache giza na kuielekea nuru, waziache na nguvu za Shetani na kumwelekea Mungu; kisha wapate msamaha wa dhambi zao, na urithi miongoni mwao waliotakaswa kwa imani iliyo kwangu mimi. MDO 26:18.

 Tutayaacha mambo ya uumbaji wa miti na matunda,tutayazungumzia tukifika mwanzo 2. Kesho tutaangalia muonekano wa Yesu kwenye mwendelezo wa MWANZO 1:14- Naamini umebarikiwa na kuna kitu umepata kitakacho kisaidia kwenye maisha yako. Pia tembelea tzworships.blogspot.com Kwa mambo mengine ya kiroho. AMEN 👏🏽👏🏽👏🏽
Axact

Tanzania Worships

Haleluyah! Karibu katika ukurasa wa Tanzania Worships ambao ni maalumu kwa ajili ya kusambaza na kulihubiri Neno la Mungu anayeishi. je kuna maoni na ushauri unataka kuuutoa ili kuhakikisha ukurasa huu unawafikia waamini na wasioamini? basi usione shaka kuwasiliana nasi kwa njia ya mitandao ya kijamii

Post A Comment:

1 comments: