SEHEMU YA 1

1 samwel 15:22(b)
"Angalia utii ni bora kuliko dhabihu."
wafilipi 2:3,8
2."msitende neno lolote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu kila mtu na amhesabu mwenzie kuwa bora kuliko nafsi yake."
8."Tena alipo onekana ana umbo Kama Mwanadamu   alijinyenyekeza  akawa mtii  hata mauti ya msalaba".
Mathayo 24:13"lakini kuvumilia hata mwisho, ndiye atakaye Okoka "


Utangulizi:
Katika Hatua za muendelezo wa ukuaji au uhimarishwaji viwango mbalimbali  vya maisha ya kiroho na kimwili, utimilifu wake umefichwa kwenye mambo  matatu ambayo ni 
UNYENYEKEVU.
 UTII.
USTAHIMILIVU. 

Utii-  ni hali kukubali kutekeleza jambo au agizo fulani unalotakiwa kufanya haijalishi litaleta matokeo hasi au chanya.

Katika maisha ya ukuaji uhimarishwaji wa fikra zetu utii ni nyenzo muhimu sana, ambayo mtu akiishi  itamsaidia kuimarika fikra na nafasi yake aliyonayo mbele za Mungu. 
1samweli 15 :22(b) tunaona umuhimu wa utii , inadhihirisha kuwa  ndani ya utii kuna kitu cha thamani ,utii ubeba na kuficha mafanikio yako ya sasa na baadae kwasababu ndani  utasaidiwa  kupambanua mambo au vitu  kulingana na mahali unako elekea. Ndani ya utii  kuna kutukuzwa /kuinuliwa  na Mungu kwenye maeneo yote aliyo ketishwa mtu. 

Tulio wengi tunashindwa kuwa watii, na hapo ndipo tunapoteza  nafasi zetu katika ulimwengu wa Roho na ulimwengu wa mwili pia. Fahamu Mungu anahitaji  mtu Mwenye roho ya utii ,kwasababu  katika kuyatimiza  mapenzi ya Mungu  kunahitajika utii ndani ya muhusika. wafilipi 2:8   Roho Mtakatifu anakukumbusha kwamba  Utii wa  Yesu Kristo  umetuletea wokovu kwa njia ya msalaba, sijui wewe utii ulio nao umeleta matokeo gani  mbele za Mungu  kwa kuzingatia nafasi uliyo nayo. 


unyenyekevu -hali ya kujishusha pasipo kuangalia haki, hadhi, au kiwango ulicho nacho kwenye eneo ulipo. Unyenyekevu  huambatana na utayari wa kujifunza mambo mbalimbali, ukiwa mnyenyekevu mbele za Mungu kuna vitu vina achiliwa ndani yako kwa lengo la kukuzidisha katika viwango  vya kufikiri na kuimarisha  misingi yako na Mungu. 

wafilipi2:3
Tunaona mtuma Paulo  anasema nasi  kuwa aliye na unyenyekevu hawez  kujihesabia haki au kuona yeye bora kuliko mwingine. 

Sikia hakikisha  una uiishi unyenyekevu  katika maisha yako yote, Fanya unyenyekevu  kuwa chakula chako cha kila siku, itakusaidia kufika mahali fulani.

Ustahimilivu - ni hali ya kuvumilia mambo au jambo kwa kipindi fulani kwa kuzingatia matokeo tarajiwa. Mtu Mwenye ustahimilivu anauwezo wa kutekeleza malengo au kusudi la Mungu lililo ndani yake kwa kiwango cha juu. Mathayo 24:13.

Inasikitisha Sana majira tuliyo nayo  watu Wengi  ndani ya mioyo yao wamepungukiwa na mambo haya matatu. 

Tafuta uso wa Bwana  mwambie akuumbie roho ya  utii, unyenyekevu na Ustahimilivu maana ndani yake kuna matokeo ya Ukomavu wa kifikra.
Mambo haya matatu ni afya mifupani kwa yeyote anayetambua na kuelewa wapi anako elekea au anapo taka kufika na Bwana,ingawa hugeuka kuwa ugonjwa kwa mtu yeyote ambaye hajui /hatambui wapi anako elekea.

Mungu akubariki Sana kwa utayari wa kujifunza. 

Axact

Tanzania Worships

Haleluyah! Karibu katika ukurasa wa Tanzania Worships ambao ni maalumu kwa ajili ya kusambaza na kulihubiri Neno la Mungu anayeishi. je kuna maoni na ushauri unataka kuuutoa ili kuhakikisha ukurasa huu unawafikia waamini na wasioamini? basi usione shaka kuwasiliana nasi kwa njia ya mitandao ya kijamii

Post A Comment:

0 comments: