ANZA SIKU NA BWANA
KWA NENO NA MAOMBI

   NENO LA MUNGU LINA NGUVU KULIKO NENO LA MWANADAMU

       MATENDO 1:8
8 Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi.
  Mpendwa jifunze;
■ Kupokea nguvu za Roho Mtakatifu.
■ Kuwashuhudia wengine habari za Yesu.
   Mpendwa,
1.Je, wewe umejazwa
   Roho Mtakatifu?
2.Je, wewe una nguvu
   za Roho Mtakatifu?
3.Je, wewe unafahamu
   utendaji wa Roho
   Mtakatifu?



TAFAKARI
  Mpendwa, watu wengine hawafahamu umuhimu wa Roho Mtakatifu ndani ya mkristo.
  👉🏽Hapa tutadondoa kidogo tu,
KAZI ZA ROHO MTAKATIFU NDANI YETU.
1.Hutuombea kwa Mungu Baba maana ndiye anayeujua moyo na mapenzi ya Mungu.
       Warumi8:26
2.Hutufanya tumtambue na kumtukuza MUNGU.
     Yohana 16:14
3:Anatuongoza katika kweli yote.
       Yohana 16:13.
4:Anatupa uwezo na ujasiri wa kuwaambia wengine habari za BWANA YESU.
     Yohana 15:26,
5:  Anatufundisha. Yeye ni mwalimu wa kila jambo/ kitu.
          Yohana 14:26.
6:Hupanda na kutoa matunda ya Roho ndani yetu.
        Wagalatia 5:18-23.
   Roho Mtakatifu ni MSAIDIZI WETU.
     Barikiwa sana mtu wa Mungu. Uwe na Jumapili njema sana.

Axact

Tanzania Worships

Haleluyah! Karibu katika ukurasa wa Tanzania Worships ambao ni maalumu kwa ajili ya kusambaza na kulihubiri Neno la Mungu anayeishi. je kuna maoni na ushauri unataka kuuutoa ili kuhakikisha ukurasa huu unawafikia waamini na wasioamini? basi usione shaka kuwasiliana nasi kwa njia ya mitandao ya kijamii

Post A Comment:

0 comments: